Friday, September 12, 2014

ASILI NA CHANZO CHA NDOA








UTANGULIZI:

I. Chanzo cha ndoa. 

A. Mawazo mbali mbali kuhusu taasisi ya ndoa ilivyoanza.
1. Hekaya ya Kiafrika (Lesotho): “Hapo kale walikuwepo vijana wanne ambao waliwinda pamoja daima. Hakuwepo mtu mwingine duniani kwa jinsi hiyo waliwaza, lakini siku moja Mungu aliumba mwanamke na akamfundisha kusema, kuoka mkate na kutengeneza vyungu, kuotesha nafaka na kupika. Hatimaye siku njema moja ndugu hawa wanne wakakutana na huyu msichana na walijiuliza, Je  huyu ni mnyama au binadamu. Mmoja wao akasema ninampenda na hivyo aliwazuia kaka zake wasimtendee kama mnyama.  Wale watatu waliondoka wakisema hitaji lao lilikuwa ni kuwinda wanyama na kama ndugu yao alimtaka mnyama yule (mwanamke)wao wangeendelea mbele kuwinda wengine kwa ajili yao. Hawakuonekana tena kwani baada ya miaka ya kuwinda walipokuwa wazee waliuwawa na simba nyikani kwa kuwa hawakuweza kujihudumia na kujilinda. Kwa upande mwingine ndugu yao aliyempenda mwanamke aliishi na yule mwanamke ndani ya pango karibu na kisima miambani. Mwanamke yule alimiliki moto hivyo alimpikia nyama, uji na mboga, ambavyo alikuwa amevilima. Mwanamume alikuwa na furaha kuu na alilishwa vema mno. Walipata watoto wengi na hata wajukuu, ambao waliwatunza katika uzee wao” (Knappert 1990: 153)
            2. Hekaya ya Kihindi: Deerghatumma ambaye ni kipofu alisema ndoa yapaswa kumpa mwanamume 
                 mamlaka juu ya mwanamke.
a. Usemi huo ulitokana na ukweli kuwa wanawake walikuwa na “mamlaka zaidi.”
b. Hata hivyo, endapo sababu ya ndoa itakuwa ni kuruhusu wanaume watumie mamlaka vibaya, ndoa yapaswa kupigwa marufuku kabisa.
            3. Wengine husema ya kuwa ndoa ilizuka tu kama vile mtu alivyozuka:
a. Yasemekana ya kuwa ndoa ni matokeo ya hitaji lihusianalo na utatuzi wa maswala ya malezi na matunzo ya watoto.
b. Kwa hiyo endapo majukumu ya ndoa yalizuka, yaweza kuendelea kuzuka na kubadilika na kuwa tofauti.
4. Endapo ndoa ni taasisi iliyoanzishwa na wanadamu, na ikiwa imetokana na hekaya au kuchipuka kwa njia ya asili tu, basi mwanadamu ana uwezo wa kubadili sheria zinazotawala ndoa au hata kuachana nayo kabisa.

B. Neno la Mungu laandika ya kuwa Mungu ndiye aliayenzisha ndoa (Mwz 2:18-25).
1. Yesu alinukuu kuhusu ndoa iliyoanzishwa na Mungu katika Math 19:5.
2. Paulo alinukuu kuhusu ndoa iliyoanzishwa na Mungu katika Efe 5:31.
3. Hivyo, hatuwezi kuibadili au kuachana nayo. Wajibu wetu ni kutii asemacho Mungu kuhusiana na taasisi yake.

C.  Kwa njia ya ndoa Mungu hutimiliza kilicho chema kwa kumpatia mwanamume msaidizi wa kumfaa.
1. “Si vema kwa mwanamume kuwa peke yake” (Mwz 2:18). Uumbaji wa mwanadamu umefanyika katika hatua mbili (Mwanzo 2 hutoa maelezo ya kina ya uumbaji wa binadamu, ambao kwanza waelezwa katika Mwz 1:26-27). Akiwa amesha muumba mwanamume, ambaye kimaumbile aliandaliwa awe na mwenzi, yamaanisha:
a. Yalikuwapo mambo zaidi ya kufanya—Kazi ya Mungu kuhusiana na mwanamume ilikuwa haijakamilika: mwanamume aliumbwa na ameumbwa kuwa na mwenzi wa kuambatana naye.
b. Mwanamume mkamilifu paradiso (mahali pakamilifu) akiwa na chakula kizuri na kazi nzuri (Mwz 2:15), na Mungu mzuri, bado hakuweza kujitosheleza yeye binafsi.
c. Binadamu aliumbwa kama kufuli na funguo—moja bila nyingine haina kazi.
d. Watu hutegemeana, sio wakujitegemea (huru)
e. Kwa asili mwanamume na mwanamke wanapaswa kuoana. Useja ni kipawa maalum kutoka kwa Mungu (1 Kor 7:7).
2. “Nitamfanyia msaidizi wakufanana naye” (Mwz 2:18).  “Msaidizi wakufanana” yamaanisha  “wa kukubaliana,” au “mwenzi” wa mwanamume, kumkamilisha na kumsaidia, sio kuwa mtumwa wake. Hii inamaanisha:
a.Mwanamume anahitaji mwenzi wa kuzungumza naye, kushiriki naye hisia, maono, furaha, huzuni, nk.
b. Uhitaji wa msaidizi kwa mwanamume wadhihirisha kuwa mwanamume anahitaji msaidizi, wakumtegemeza, mshiriki, rafiki.       
c. Mwanamume anahitaji msaada ili kuijaza nchi na katika jukumu la kuitiisha  nchi.
d. “Msaidizi” ni cheo cha kuheshimika.
(1) Mungu mwenyewe wakati mwingine huitwa “Msaidizi” (Zab 30:10; 40:17; Ebr 13:6).
(2) Yesu alimwita Roho Mtakatifu “Msaidizi” wetu (Yoh 14:16, 26; 15:26; 16:7).
(3) Endapo cheo “Msaidizi” ni chakumstahili muumba wa ulimwengu, basi hakiwezi kuwa na hadhi ya chini kwa mke. Kinyume chake, ni cheo cha heshima,  na mke ajivunie kuwa nacho.
(4) Mume na mke wautazame Utatu unao “saidiana” kuumba, kutawala, kufurahia, kuhuzunika, nk.
3. Mchakato aliotumia Mungu wa kumpa Adam jukumu la kuwapa wanyama majina ulidhihirisha wazi kuwa hakuwepo mnyama aliyefaa kuwa msaidizi wa  mwanamume (Mwz 2:19-20).
a. Bwana akamletea Adamu wanyama awape majina, yamaanisha,kutathmini sifa na ubora wao. Adamu alitathmini sifa na ubora wao na kutokana na hizo akawapa majina yaliyowastshili. Na mchakato huo ulidhihirisha kuwa “hakuwepo msaidizi wa kufanana naye” (Mwz 2:20).
b. Rabi Fulani anatupa picha hii—wanyama wanakuja kwa jozi: “Kila mmoja ana mwenzi, ila mimi sina mwenzi.”
c. Huenda Adamu alishayagundua mahitaji yake ya ndani kutokana na jinsi Mungu alivyomuumba—hitaji la mwenzi, usaidizi katika majukumu ya kimaisha, hitaji la binafsi la kujamiiana. Hata hivyo, Adamu hakupata alichokihitaji miongoni mwa wanyama kwani alichohitaji si mnyama.
                        d. Matumizi: Wanaume, je mmeshatambua na kukubali kuwa hamjitoshelezi?
(1) Uliumbwa kwa namna ya kuwa tegemezi kwa mkeo.
(2) Wapaswa pia kujua hitaji lako la msaidizi haliwezi kutoshelezwa na chochote kile miongoni mwa vitu au wanyama.       

D. Mungu alimuumba msaidizi wa kumfaa mwanamume kutokana na mwili wa mwnamume (Mwz 2:21-22).
1. Mungu alimuumba msaidizi wakati Adamu amelala. Kumbukumbu hazionyeshi kuwa Adamu alihusika kwa namna yoyote katika mchakato wa uumbaji.
2. Adamu hakujua namna ya kutatua hitaji lake la msaidizi.
3. Kutokana na kusudi lake la milele na hekima yake Mungu alilitambua hitaji la Adamu hasa. Ni yeye pekee ajuaye vigezo vilivyosababisha mwanamke awe msaidizi wa kufaa, mwenzi, rafiki na mshiriki kwa mwanamume ili ile sura ya mfano wa Mungu ionekane ndani yao.
4. Bwana huamua namna ya kukidhi hitaji- nini kinafaa kuwa msaidizi wa mwanamume.
5. Mungu alimuumba msaidizi kwa kutumia sehemu ya mwili wa Adamu, ubavu wake, mwili ambao ni tofauti na ule wa wanyama. Inamaanisha:
a. Hapaswi kufananishwa na jamii ya wanyama.
b. Yeye si hayawani mwenye kutulemea, licha ya tamaduni nyingi kuwachukulia wanawake 
     kwa namna hiyo.
c. Hapaswi kupigwa, kwa viboko au maneno.
6. Kama alivyosema mwenye hekima mmoja, “Mwanamke hakutokana na sehemu ya kichwa cha mwanamume, asije akamtawala, au hakutokana na sehemu ya miguu,asije kanyagwa naye, lakini katoka ubavuni ili awe mshiriki kama mwenzi aliye sawa naye ingawaje ana jukumu tofauti.”
            7. Matumizi: Mwenendo na tabia yako kwa mume au mke wako ikoje?

II. Asili na kusudi la ndoa.

A. Kwa asili, ndoa ni ya kiroho.
1. Ndoa yawakilisha umoja kati ya washiriki watatu wa Utatu Mtakatifu (Baba, Mwana, Roho Mtakatifu). Kama vile washiriki watatu wa Utatu Mtakatifu walivyo nafsi tofauti bali Mungu mmoja, vivyo mume na mke ni watu tofauti bali wameunganishwa na “kuwa mwili mmoja” (Mwz 2:24).
2. Ndoa ni mfano wa uhusiano wa Yesu na kanisa lake (Efe 5:22-33).
            a. Mke na amtii mumewe kama kanisa linavyomtii Kristo.
            b. Mume na ampende mkewe kama Kristo alivyolipenda kanisa akajitoa kwa ajili ya kanisa .
c. Kwa hiyo, wana ndoa wanapaswa kuwa mfano ulio hai na wazi wa uhusiano wa Kristo na kanisa lake.


B. Ndoa ni taasisi ya msingi na kiini cha jamii ya wanadamu.          
            Kuvunjika kwa ndoa (kupitia talaka,muunganiko wa jinsia moja, na kujamiiana nje ya ndoa), ambavyo hutokana na kutofuata neno la Mungu, huharibu utamaduni wa watu wa Magharibi na utafanya yayo hayo kwa utamaduni wa watu wasio wa ki-Magharibi.

C. Kusudi la ndoa:
1. Kutokana na Mwanzo makusudi yafuatayo ya ndoa hujitokeza:
            a. Urafiki (Mwz 2:18).
            b. Umoja (Mwz 2:24).
            c. Uzao (Mwz 1:28; 9:1, 7).
            d. Starehe (Mwz 3:16; tazama pia Mhu 9:9; Wimbo ulio Bora 1-8; 1 Kor 7:3-5).
2. Pamoja na hayo Agano Jipya laongezea makusudi yafuatayo ya ndoa:
a. Ulinzi dhidi ya uasherati (1 Kor 7:9).
b. Utakaso wa kibnafisi au unaoendelea (Efe 5:26).

BY JONATHAN MENN

jonathanmenn@yahoo.com